
Polisi na baadhi ya wanakijiji wakiwa eneo la tukio
Kufuatia tukio hilo watu sita wanashikiliwa na polisi akiwemo Mwenyekiti na Afisa Mtedaji wa kijiji hicho cha Kisharita kilichopo wilayani Iramba.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Stella Mutabihirwa baada ya kutokea kifo hicho cha Agnes, wananchi kwa kushirikiana na Mwenyekiti na Mtendaji wa kijiji waliwakamata wanawake hao watatu na kuwafungia nyumbani kwa Mwenyekiti wa kijiji hicho.
Inadaiwa kuwa mara baada ya kutoka kwenye mazishi, wananchi wakiongozwa na Mtendaji wa kijiji waliwahoji wanawake hao kuhusiana na kifo cha kabla ya kuwauwa kwa kuwachoma moto.