
Picha kutoka eneo la tukio
Ajali hiyo imehusisha Fuso yenye namba za usajili T 239 AFD lililokuwa limebeba bidhaa za sokoni kutokea Wilaya ya Lushoto kwenda Handeni.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa kwa taarifa za awali watu 4 ndio waliopoteza maisha na baadaye waliongezeka wengine wawili ambao walikuwa majeruhi.
"Waliotutoka mwanzoni walikuwa wanne lakini wameongezeka majeruhi wawili na jumla kufikia 6 ambapo kati yao waliofariki wanaume ni 4 na wanawake ni wawili," amesisitiza Kamanda Jongo.