
Russell Westbrook akimpita mlinzi wa timu ya Denver Nuggets kwenye mchezo wa NBA wa mzunguko wa pili.
Westbrook sasa amefikisha jumla ya ‘Triple-double’ 177 tokea aanze kukipiga kwenye NBA mwaka 2008 na kufukuzia rekodi ya kufikisha ‘Triple-double’ 181 inayoshikiliwa na Oscar Robertson kwenye historia ya NBA tokea ‘Triple-dpouble’ zilipoanza kuhesabiwa mwaka 1951.
Nyota huyo aliye kwenye kiwango bora kwa sasa amebakisha michezo 9 kuifukuzia rekodi hiyo wakati ambao NBA inakaribia kumaliza mzunguko wa pili wakiwa kwenye nafasi ya 10 kwa upande wa Magharibi kabla ya kuelekea kwenye michezo ya ‘NBA Play-in’ Mei 18, 2021.
Rekodi nyingine zilizowekwa na Westbrook msimu huu, ni pamoja na kukamilisha kuzifunga 'Triple-double' timu zote 30 za NBA pamoja na kupiga 'Multi-Triple-double' nyingi za zaidi ya alama 30, rebaundi 10 na assiti 10.