Miquissone akishangilia goli dhidi ya Al Ahly
Goli pekee la Simba SC kwenye mchezo huo limefungwa na winga Luis Miquissone dakika ya 32 baada ya kupiga shuti kali.
Ushindi huo umeifanya Simba SC kuongoza Kundi A baada ya kufikisha pointi 6 kwenye michezo miwili ya kwanza.
Nafasi ya pili inashikiliwa na Al Ahly yenye pointi 3, nafasi ya tatu ni AS Vita yenye pointi tatu baada ya kupata ushindi wa goli 4-1 dhidi ya Al Merrick.