Tuesday , 20th Oct , 2020

Wafanyabiashara wa soko la Tabata Muslim wameiomba serikali kuwaboreshea miundombinu ya soko hilo ili waweze kufanya biashara vizuri hasa wakati wa mvua kutokana kuvuja kwa baadhi ya mabanda.

picha ya soko la Tabata Muslim

Wakizungumza na kurasa  hii leo wamesema soko hilo ni la muda mrefu licha ya kuwa ni soko kubwa  lakini haliboreshwi na halmashauri imekua hailizingatii na kudai kuwa baadhi ya maeneo katika soko hilo yamerekebishwa na fedha zao pamoja misaada ya watu wengine.

Aidha Wafanyabiashara hao wamesema kuwa changamoto nyingine ni pamoja na maeneo lilipo soko hilo ambalo lipo nyuma ya kituo cha mafuta hivyo wakati mwingine kukosa wateja kutokana na kuwepo katika eneo lililojificha.