Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
Akizungumza na EATV&EA Radio Digital, Lema amesema kuwa kutokana na hayo yote zipo hatua ambazo kama chama wamepanga kuzichukua ili kuhakikisha mateso kama hayo ndani ya chama chao yanakwisha.
"Niliposikia kauli ya Mambosasa imenishangaza, nafikiri sasa shetani anaweza kuja kujifunza tuition ya uongo duniani, kitendo walichofanyiwa akina Halima, Ester na Jesca ilibidi wanawake wote nchi nzima wapige kelele" amesema Lema.
Wabunge Ester Bulaya, Halima Mdee na Jesca Kishoa, wamelazwa katika Hospitali ya Agakhan, kufuatia majeraha waliyoyapata kwa kile kilichoelezwa kuwa walipigwa na Polisi.



