Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Jonathan Shana
Akizungumza leo Machi 10, 2020, na EATV&EA Radio Digital, Kamanda wa Polisi mkoani humo Jonathan Shana, amesema kuwa ndani ya Mkoa wake, hakuna tukio la namna hilo na kwamba Sabaya ni kiongozi muadilifu.
"Kwa kawaida mtu akipigwa risasi ama kujeruhiwa anapaswa kutoa taarifa kituo chha Polisi, hata mimi baada ya kuona hizo taarifa zinasambaa, nimetafuta katika vituo vyangu vyote hakuna, kwahiyo sisi hatuna taarifa kama hiyo kwenye vituo vyetu" amesema Kamanda Shanna.


