
Afisa habari wa TFF Boniface Wambura amesema kuwa wikiendi hii ligi kuu kutakua na mechi 5 ambapo kesho kutakuwa na michezo mitatu Coastal Union itaumana na Ashanti United kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Ruvu Shooting itaikaribisha Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwania wakati Mbeya City itacheza na Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Mechi za Jumapili (Machi 9 mwaka huu) ni Tanzania Prisons na Simba kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, na JKT Ruvu na Mtibwa Sugar zitacheza Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.