Tuesday , 16th May , 2017

Rais wa Manzese 'Madee Seneida' amewauliza  watu wanaojiombea kifo kutokana na ugumu wa maisha kwa madai wamechoka kuishi wanataka kupumzika, je mema gani wametenda ili wakifa wakapumzike.

Madee kupitia ukurasa wake wa Twitter amehoji kama kuna watu wanahitaji kufa ili wakapumzike ni mema gani wametenda huku kweye ukurasa wake wa Instagram akiongeza kwamba "unakaba,unasengenya,unadhulumu, alafu unaomba ufe ukapumzike! JIPANGE" - Madee ameandika.