Madee (Kushoto) akiwa na Fid Q ndani ya FNL ya EATV
Madee anasema ukimtoa Fid Q wasanii wengine ambao anawakubali na kupenda kazi zao kutoka Bongo ni pamoja na Mzee wa Dume Suruali Mwana FA, Mr Blue, Roma Mkatoliki pamoja na God Zillah.
Mbali na hilo Madee anasema yeye amejiwekea utaratibu wa kubadili aina ya muziki wake kila baada ya miaka mitano, ili kwenda sawa na soko la muziki la wakati huo na kusema ameamua kufanya hivyo sababu muziki wa sasa unahitaji ujanja ujanja ili mambo yaweze kwenda.