
Mwenyekiti wa AWATA Andrew Kapelela amesema, mashindano ya Nyerere Cup yaliyokuwa yakishirikisha nchi za Burundi, Uganda, Kenya na Congo yameahirishwa kutokana na mazingira yaliyo nje ya uwezo hivyo watapanga tarehe maalumu kwa ajili ya mashindano hayo.
Kapelela amesema, mashindano ya klabu bingwa ambayo hivi sasa yapo mbele yao yatashirikisha vilabu mbalimbali vya Tanzania ambavyo vinaamini vina uwezo wa kushiriki.