mkali wa miondoko ya Hip hop nchini Tanzania Bonta Maarifa
Bonta amewataka mashabiki kuelewa kuwa wasanii wana haki zote za kusimama upande wowote kisiasa wakiwa kama raia wengine wa kawaida.
Mkali huyo pia ametaka wasanii hao kufahamu tofauti zao kama raia wa kawaida, na katika nafasi zao kama wasanii ambao wana kundi kubwa la watu nyuma yao wenye mitizamo tofauti, kitu ambacho kwa namna moja ama nyingine kinazua athari kwa kundi lile la watu ama mashabiki.


