Friday , 28th Aug , 2015

Mrembo anayeshikilia taji la Miss Tanzania kwa sasa, Lilian Kamanzima amefungua moyo wake kueleza namna ambavyo imekuwa changamoto kwa upande wake, kushikilia taji hilo katika kipindi ambacho mashindano hayo yalifungiwa.

Mrembo anayeshikilia taji la Miss Tanzania 2014, Lilian Kamanzima

Lilian akiwa na matumaini mapya kwa mambo kubadilika kufuatia hatua mpya zilizochukuliwa kuyanusuru mashindano hayo
ameieleza eNewz kuwa katika kipindi chote amejitahidi kutimiza majukumu aliyotakiwa kama Miss Tanzania, huku akiendelea pia na masomo yake, kujiondoa kwa wadhamini kukiwa pia ni pigo jingine ambalo limesababisha wakati mgumu katika kipindi ambacho ametumikia taji hilo.