
Mshambuliaji wa Yanga Heritier Makambo.
Rekodi ya timu hizo mbili inaonesha tangu timu ya Stand United ipande ligi kuu msimu wa 2014/15, zimecheza mechi 8 ambapo Stand United imeshinda mechi 1 pekee huku Yanga ikishinda mechi 7.
Timu hizo zilikutana kwa mara ya kwanza tarehe 25/10/2014 ambapo Yanga ilishinda mabao 3-0. Kisha zikakutana tarahe 21/04/15 na Yanga ikashinda 3-2.
Msimu wa 2015/16 zilikutana tarehe 09/12/2015 ambapo Yanga ilishinda mabao 4-0 kabla ua kushinda tena mabao 3-1 kwenye mechi iliyopigwa tarehe 03/05/2016.
Katika msimu wa 2016/17 Stand United ilipata ushindi kwa mara ya kwanza dhidi ya Yanga ikifunga bao 1-0 kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Kambarage Shinyanga. Timu hizo tena zikakutana msimu huo ambapo Yanga ilishinda mabao 4-0.
Msimu uliopita wa 2017/18 Yanga ilianza kwa kushinda mabao 4-0 kabla ya mechi ya pili kushinda 3-1. Mchezo wa leo utapigwa saa 10:00 jioni. Yanga imeshacheza mechi moja na kushinda huku Stand United nayo ikicheza mechi mbili na kushinda zote.