Friday , 8th Jan , 2016

Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), limetuma salamu za rambirambi kwa kocha msaidizi wa Taifa Stars Hemed Suleiman “Morocco” kufutia kifo cha baba yake mzazi Suleiman Ally Hemed kilichotokea juzi kisiwani Zanzibar.

Shirikisho la kandanda Tanzania TFF

Katika salamu hizo za rambirambi, TFF imewapa pole wafiwa, ndugu jamaa na marafiki na kusema wapo pamoja na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Aidha pia TFF imetuma rambirambi (ubani) wa shilingi laki mbili (200,000) kwa familia ya kocha Hemed Moroco kufuatia kifo cha baba yake Suleiman Ally.

Mazishi ya marehemu Suleiman Ally Hemed imefanyika jana jioni mjini Zanzibar