Kikosi hicho kinachojiandaa na mechi ya kuwania kufuzu kucheza michuano ya mataifa ya Afrika Septemba 5 mwaka huu kimemuacha mlinda mlango huyo kutokana na kuwa majeruhi.
Katika taarifa yake kocha wa Stars Charles Boniface Mkwasa amesema wachezaji wakulipwa wa Tanzania wote watajiunga na Stars kulingana na kalenda ya FIFA pindi itakapohitaji wachezaji wa vilabu kwenda kuzitumikia timu zao za taifa.




