Ismail Gambo ‘Kussi' (Kushoto ) na Omary Wayne (Kulia) waliochukulia na Majimaji kwa mkopo wakitokea Azam Fc
Wawili hao matunda ya "Academy" ya mabingwa hao wa Afrika Mashariki na kati tayari wamesafiri kwenda Songea kujiunga na Majimaji iliyorejea ligi kuu ya soka Tanzania Bara msimu huu.
Wawili hao wanafanya idadi ya wachezaji watatu ndani ya wiki moja kutolewa kwa mkopo Azam FC, baada ya winga Joseph Kimwaga kupelekwa Simba SC wiki hii.




