
Katibu Mkuu wa Chama cha mpira wa Magongo mkoa wa Dar es Salaam DRHA Mnonda Magani amesema, ligi hiyo iliyoanza kutimua vumbi wiki iliyopita imekuwa na muitikio mkubwa kwa mashabiki mbalimbali kujitokeza.
Kwa upande mwingine Magani amesema, katika ligi mbalimbali zilizopita kulikuwa na tatizo la timu shiriki kuchelewa kufika uwanjani hali iliyokuwa ikipelekea timu kufutiwa pointi lakini kwa msimu huu wamefanikiwa kutatua tatizo hilo kwa kupanga ratiba ambayo imesaidia timu zote kufika kwa muda unaotakiwa.