Friday , 27th Nov , 2015

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania Bara The Kilimanjaro Stars Abdallah Kibaden amesema, watacheza kwa tahadhari katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi hapo kesho dhidi ya Ethiopia ili kuweza kutunza nguvu kwa ajili ya robo fainali.

Kibaden amesema, wanajua Ethiopia wanataka sana ushindi ili waende robo fainali lakini kwa upande wa kikosi chake.

Kili Stars imejihakikishia robo fainali baada ya ushindi mfululizo katika mechi mbili za awali 4-0 dhidi ya Somalia na 2-1 dhidi ya Rwanda na hapo kesho kukamilisha mechi zake za kundi A ikiwa kileleni.