Monday , 20th Jun , 2016

Kocha wa Timu ya JKT Ruvu Abdallah Kibeden amesema, anaamini kikosi cha JKT Ruvu kwa msimu ujao kitaleta ushindani kwani anaanza nacho na atahakikisha anakijenga ili kuwa imara.

Kocha wa JKT Ruvu, Abdallah Kibaden

Kibeden amesema, wameshaanza maandalizi ya kujenga kikosi na anaendelea kuangalia kikosi cha vijana cha chini ya miaka 20 na watahakikisha wanasimama imara kupata wachezaji wazuri, wenye nidhamu ya hali ya juu na kuifikisha timu pale wanapopahitaji.

Kibaden amesema, katika zoezi zima la usajili hawagombanii wachezaji na wala wahategemei wachezaji walioachwa na vilabu vingine ndipo wawachukue kwani wanaangalia nidhamu na uwezo wa mchezaji kwani ndivyo vitaiweka timu katika nafasi wanayoihitaji wao.