Tuesday , 17th May , 2016

Kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana cha Tanzania Serengeti Boys hii leo kinashuka kucheza mchezo wao wa pili dhidi ya wenyeji India katika michuano ya kirafiki ya vijana Uwanja wa Tilak Maidan, Vasco, Goa nchini India.

Kikosi cha Serengeti Boys na Marekani kikiwa Uwanja wa Tilak Maidan, Vasco, Goa nchini India katika mchezo dhidi ya Marekani

Kocha wa Serengeti Boys Bakari Shime amesema, hali ya hewa kwa upande wao ni nzito kwani ni joto sana lakini haikuwafanya washindwe kufanya vizuri katika mchezo wa awali ningawa hawakuweza kushinda lakini walitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya taifa ya vijana ya Marekani.

Shime amesema, vijana wake wamejiandaa kwa ajili ya kupambana katika mchezo wa leo na hali ya hewa haitoweza kuwaathiri na wanaamini watarudi na faida mara baada ya kukamilika kwa michuano hiyo.

Shime amesema, mchezo wa awali umewajenga wachezaji wake na wanajua umuhimu wa mchezo wa leo na wanajiamini kuwa wanauwezo wa kucheza na timu yoyote.