Wednesday , 10th Feb , 2016

Mwanamuziki kutoka nchini Kenya na ndani ya kundi la Necessary Noize, Naziz ametikisa mitaa ya Kenya baada ya kuonesha nguvu kubwa kwenye ujio wa ngoma yake aliyoipa jina la 'Wedding Ring'.

NAZIZI

Wimbo huo ambao anategemea kuuachia siku ya wapendanao 'Valentine', umeanza kutangazwa na msanii huyo kwa namna ya kipekee ambapo ameweka matangazo ya wimbo wake huo kwenye mabango makubwa ya matangazo 'Billboards' kitu ambacho hakijawahi kutokea kwa masanii yoyote nchini humo.

Kupitia akaunti yake ya Instagram Naziz amejigamba kwa kuonesha kuwa yeye ndiye mwanamuziki pekee nchini kwao kuweka matangazo ya wimbo wake kwenye mabango makubwa barabarani, ikiwa ni ujio wake wa kishindo baada ya ukimya wa muda.