Tuesday , 10th Feb , 2015

Mwimbaji wa miondoko ya injili nchini, Emmanuel Mbasha hatimaye amefunguka juu ya mtoto ambaye mkewe Flora Mbasha amejifungua na kuweka wazi kuwa, kwa sasa asingependa kusema chochote juu yake mpaka pale wakati muafaka utakapofika.

Mwimbaji wa muziki wa injili nchini Tanzania Emmanuel Mbasha

Mbasha katika mahojiano maalum na eNewz ameongezea kuwa, Mama wa Mtoto vilevile ndiye mtu sahihi wa kueleza ukweli juu ya ni nani baba halisi wa mtoto, huku kwa upande wake akisema ni mapema mno kulizungumza suala hili.