Tuesday , 24th Feb , 2015

Tamasha kubwa lenye lengo la kutangaza sanaa na utamaduni wa kiafrika lijulikanalo kama "Karibu Music Festival”, limetangaza kukaribisha maombi ya wasanii watakaopenda kushiriki katika tamasha hilo kwa mwaka huu.

Karibu Music festival

Zoezi la maombi ya kushiriki katika tamasha hilo linafanyika kwa njia ya mtandao likihusisha wasanii wale wanaofanya muziki wa Live.

Karibu Music Festival ambayo pia hutoa nafasi ya mafunzo kwa watakaoshiriki, kwa mwaka 2015 itafanyika kwa siku tatu mfululizo kuwanzia tarehe 6 mpaka 8 mwezi Novemba 2015 na kuhusisha wasanii kutoka ndani na nje ya Tanzania.