Wednesday , 20th May , 2015

Msanii wa Bongo Heri Muziki ambaye anafanya miondoko ya R&B, amesema kuwa baada ya kumaliza shule ambayo ilikuwa ikichukua sehemu kubwa ya muda wake, kwa sasa amekuwa na muda zaidi wa kufanya muziki akiwa tayari na rekodi za kutosha.

msanii wa miondoko ya bongofleva nchini Heri Muziki

Staa huyo amekazia kuwa, elimu ndiyo kitu ambacho anakizingatia zaidi mbali na muziki, amesisitiza pia kuwa, bado ana mpango wa kujiendeleza zaidi kielimu, fani yake kubwa ambayo amejikita ndani yake ikiwa ni Biashara.