Thursday , 7th May , 2015

Msanii wa muziki Cyrill Kamikaze amewataka wadau wa muziki kuangalia nguvu ambayo msanii hutumia kuwekeza katika kazi yake, na kuipa sapoti kwa kiwango kile kile alichonacho.

msanii wa bongofleva nchini Kamikaze

Staa huyo amesema kuwa, kitendo cha kupuuza ama kulinganisha kazi ya msanii ambayo ametumia gharama ya kawaida kuifanya, na zile ambazo msanii husika anakuwa amewekeza mamilioni, kunamkatisha tamaa yule anayewekeza zaidi na hivyo kuondoa viwango ama ubora katika kazi zao.