
Wasanii hawa wametakiwa kuendeleza moyo wao katika kazi zao na pia kuendelea kuwa mfano mzuri kwa jamii, hususan wanawake ambao kwa asilimia kubwa hujiweka nyuma kutokana na hofu na pia kutokujiamini kutokana na jinsia yao.
Pongezi hizi zinafuatia tukio la Anne pamoja na Juliana kupatiwa tuzo ya kutambuliwa mchango wa mwishoni mwa wiki kutoka kampuni maarufu huko Uganda, katika msimu huu wa mwezi wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.