
AY akiwa kwenye Kontena ambalo aliishi mwaka 1999
Fid Q ambaye bado yupo kwenye fungate la 'Honey Moon' baada ya kufunga ndoa wiki hii, amemshauri mkongwe mwenzake huyo alinunue Kontena hilo kisha atengeneze Studio kwaajili ya wasanii wanaotoka mikoani.
''Nimemshauri AY alinunue lile Kontena kisha aligeuze studio na kijiwe maalum kwa ajili ya wasanii wote wanaotoka mikoani na kuja dar Kwa ajili ya kuendeleza harakati zao za sanaa'', ameeleza Fid Q.
Jana kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii AY aliweka wazi kuwa alikuja Dar es salaam mwaka 1999 kwaajili ya kuendeleza kipaji chake lakini hakuwa na pakufikia ikabidi awe analala kwenye Kontena moja maeneo ya Upanga.