Tuesday , 25th Mar , 2014

Msanii Daddy Owen wa nchini Kenya, baada ya kushuhudia mafanikio makubwa kupitia muziki
anaofanya, ameamua kusherekea na mashabiki kwa namna yake kupitia mashindano makubwa ya mpira wa miguu ambayo atayaandaa hivi karibuni.

Daddy Owen

Daddy Owen ambaye pia yuko katika mpango wa kuoa mwishoni mwa mwaka huu, amesema kuwa, michuano hii ya mpira wa miguu atakayoianzisha hivi karibuni, itawapatia nafasi wapenzi wa mchezo huu kuhudhuria na kupata burudani ya kutazama kabumbu moja kwa moja na bure kabisa.

Daddy Owen amesema kuwa, uamuzi hii ni kufuatia suala lililo wazi kuwa, mchezo wa mpira wa miguu umekuwa na mashabiki wengi, ila asilimia kubwa wanashindwa kupata nafasi ya kuuona mchezo huu moja kwa moja kutokana na gharama za kiingilio ambazo hawazimudu.

Tags: