Friday , 18th Sep , 2015

Star wa muziki Belle 9, amezungumzia tabia ya wasanii kuanika maisha yao binafsi katika vyombo vya habari ikiwepo mapenzi, kwake hii ikiwa si sawa na akiwa haamini kama inaweza kumsaidia kivyovyote msanii kusimama kimuziki.

Staa wa muziki Belle 9 akiwa na mrembo

Belle 9 amesema kuwa, hiyo inatokana na kujali pia familia yake ambayo imemlea katika misingi ya dini akiamini kabisa kuwa kuna mambo akiyafanya yanawagusa moja kwa moja, neno lake kwa wasanii wengine pia likiwa ni kuweka muziki mbele na mambo binafsi kwa ajili yao binafsi.

Kwa kuanzia na kwa kutathmini hali halisi katika soko la muziki Bongo, hapa Belle 9 anafunguka juu ya tabia hiyo.