
Zitto Kabwe
Zitto ambaye ameambatana na Mbowe katika mkutano wake na wanahabari leo mjini Dodoma, amesema kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kumtaja Mbowe katika sakata la dawa za kulevya ni sawa na kutangaza vita na chuki dhidi ya chama hicho.
Amesema kuichafua CHADEMA ni sawa na kuuchafua upinzani hivyo na yeye hawezi kukaa kimya kuona upinzani ukishambuliwa, na ndiyo sababu ya kuongeza nguvu kwa kuungana naye.