
Picha kivuli ya watu wakiperuzi mtandaoni.
Wakitoa maoni yao kupitia Ukurusa wa FaceBook wa East Africa Television ambapo tuliuliza juu ya hasara au kero apatazo mtumiaji wa mtandao huo, wengi wamependekeza kuongezwa kwa vipengele mbalimbali vinavyoweza kudai ruhusa ya mtumiaji ili kutoa au kupokea taarifa, kadhalika na kuchukuliwa kwa vitu vyao kama picha ya utambulisho 'Profile Picture' na namba ya mtumiaji.
Pia utaratibu wa mtandao huo kuruhusu watu kwenye makundi yanayoundwa kuongezwa bila ridhaa ya mtu umelalamikiwa, hivyo kuhitaji angalau uwepo utaratibu wa mtu kukubali au kukataa pindi anapoongezwa kwenye kundi.
India kupitia kwa Waziri wa Teknolojia Bw. Ravi Shankar Prasad, wamelalamika juu ya mtandao huo kushindwa kudhibiti au kufuta kabisa ujumbe ambao unakuwa si wa kweli na unasambazwa kwa haraka kwa watu wengi wa eneo moja ambao mwisho husababisha madhara kama vifo.