Thursday , 29th May , 2014

Jeshi la polisi limewakamata na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa 16 wakiwemo 9 wa milipuko ya bomu katika baa moja Arusha.

Baadhi ya watuhumiwa akipelekwa Mahakani mjini Arusha

Jeshi  la  polisi  nchini  limewakamata  na  kuwafikisha mahakamani  watuhumiwa  16  wa  uhalifu  9  kati  yao wakihusishwa   na  tukio  la  milipuko  ya  bomu  katika  baa  ya Night park  jijini   Arusha  na  wengine  wa wakijihusisha  na vikundi vya uhalifu  vya  ndani na nje  ya  nchi .

Mkurugenzi   wa   makosa  ya  jinai  nchini  kamishna  Isaya Mgulu amesema  kwenye kundi hilo   watuhumiwa     sita  wanakabiliwa na   tuhuma  za  kukusanya  na  kusafirisha vijana  nje  ya nchi kwa  lengo  la  kujifunza uhalifu   na  mmoja   kwa tuhuma  za kufanya  udanganyifu  wa  kupata hati  ya  kusafiria.
 
Kamanda mgulu  amesema  watuhumiwa  9  wanaohusishwa na mlipuko  wa  bomu katika  baa ya nightpark  wanakabiliwa  na makosa  ya  jinai  yakiwemo  ya  kuua  na  kujeruhi  na watuhumiwa   sita    pia  wanakabiliwa  na  makosa  ya  jinai yakiwemo   kushawishi  na  kuwasafirisha  vijana   kujiunga na vikundi  vya kigaidi   ambapo   tayari   imeelezwa   kwamba   walishawasajili    vijana   17   kwa    ajili    ya   kujiunga   na  vikundi hivyo.

Baada  ya  taarifa  ya  DCI  watuhumiwa  hao   walipandishwa kizimbani  katika  mahakama ya hakimu mkazi  mkoani  Arusha  na kusomewa  mashtaka  17   ambapo watuhumiwa    nane  kati ya  16 wamesomewa  mashtaka ya mauaji, watuhumiwa     saba    wakisomewa  mashtaka  kupanga  na  kuhamasisha  vijana kujiunga na  vikundi  vya ugaidi   na  mmoja  akishtakiwa  kwa kufanya udanganyifu  wa  kupata  hati  ya  kusafiria.

Baada  ya kusomewa  mahstaka  hayo  na   hakimu  Mustafa Siani    akisaidiana  na  mwendesha mashtaka  wa  serikali Maselina  Mwamunyange  watuhumiwa   15  wa  kesi  za  jinai  hawakutakiwa  kujibu  lolote,  wakati mtuhumiwa  mmoja  wa kosa  la  udanganyifu   wa  hati   alikana  shitaka  linalomkabili .

Watuhumiwa  wote  wamepelekwa  rumande   na  kesi  ya watuhumiwa  wa  kushawishi  vijana  kujiunga na vikundi  vya ugaidi  itatajwa  tarehe  Juni  11 mwaka huu  wakati  wanaokabiliwa   na  shitaka   la       mauaji    inatarajiwa   kutajwa tarehe  12 Juni 12 mwaka huu.