Monday , 22nd Jul , 2019

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao, amethibitisha kupokea taarifa ya vifo vya watu sita huku wengine 22, wakijeruhiwa kutokana na ajali iliyohusisha gari aina ya Toyota hiace na Land Cruiser, iliyotokea Julai 21, majira ya 1:00 usiku, katika eneo la Nyambuka Wilaya ya Ka

ACP Abwao ameeleza chanzo cha ajali hiyo kuwa, ni mwendo kasi wa dereva wa Hiace iliyokuwa na abiria ikitokea Kakola kwenda Kahama mjini, na kwamba barabara hiyo imekuwa na vumbi nyingi.

''Barabara ya Kakola,  Kahama imekuwa na vumbi nyingi,  kwasababu imekuwa ikitumiwa na  magari mengi hii ni  baada ya kuibuka kwa machimbo mapya ya Kakola Namba 9'' amesema ACP Abwao.

Aidha Kamanda Abwao amesema, baadaye leo atatoa taarifa rasmi za ajali hiyo, ikiwemo majina sahihi ya watu waliopoteza maisha na majeruhi wa ajali hiyo.