Sunday , 27th Nov , 2016

Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Bw. Sergei Lavrov amezikosoa nchi za Magharibi kwa kile alichodai kuwa ni kufumbia macho vitendo vya makundi ya kigaidi vya kutumia silaha za kemikali nchini Syria.

Bw. Lavrov amesema ametahadharisha kuwa ukimya huo wa nchi za magharibi kuhusu utumiaji wa silaha za kemikali ni sawa na kubariki na kuwaruhusu magaidi hao wafanye kila aina ya uhalifu wa kivita.

Katika maelezo yake, Bw. Lavrov ametahadharisha juu ya mwenendo wa sasa wa nchi hizo wa kuendelea kuyaunga mkono makundi ya kigaidi huku akitaka ufanyike uchunguzi kuhusu utumiaji wa silaha za kemikali nchini Syria.

 

________________
Kumpigia KURA msanii unayempenda kwenye #EATVAwards Bofya hapa https://www.eatv.tv/awards