
Wakimbizi wakisajiliwa katika kambi ya Kavumu
Mwakilishi mkazi wa UNHCR Burundi Abel Mbilinyi, amesema kuwa tume hiyo inatokana na ushauri wa Msaidizi wa Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR Volker Turk aliyefanya ziara nchini Burundi juma moja lililopita.
Kadhalika Mbilinyi anaeleza namna tume hiyo itakavyoepuka mambo ya kisiasa na kujikita katika utendaji kwa kutumia weledi na pindi mambo yatakapokuwa juu ya uwezo wao wataishauri serikali yao kuchukua hatua stahiki.