Thursday , 20th Nov , 2014

Chama cha wafanyabiashara wa viwandani na kilimo (TCCIA) kimetoa wito kwa wafanyabiashara kote nchini kuitumia vizuri wiki ya mlipa kodi inayoendelea nchini ili waweze kupata elimu ya kutosha kuhusiana na faida za kulipia kodi.

Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Dodoma, Faustine Mwakalinga

Wito huo umetolewa leo na mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Dodoma, Faustine Mwakalinga wakati akizungumza na East Afrika Radio kuhusiana na faida za wiki ya mlipa kodi kwa wafanyabiashara nchini.

Mwakalinga amesema kuwa elimu inayotolewa na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kuhusiana na umuhimu wa kulipa kodi ina faida kubwa kwa wafanyabiashara hata kwa wale ambao wanakwepa kulipa kodi kwani wakipata elimu ya kutosha wanaweza kuanza kulipa kodi kwa ajili kukuza uchumi wa Taifa.

Pia ametoa wito kwa Jumuiya za wafanyabiashara kuhakikisha kuwa zinatatua matatizo yao na serikali kwa kukaa mezani na kuachana na migomo isiyokuwa na tija kwa taifa.