Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Lenard Subi
Takwimu hizo zimetolewa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Lenard Subi wakati wa ufunguzi wa ofisi ya shirika la kimataifa la world lung foundation, linalojishughulisha na uboreshaji afya ya mama na mtoto
Dkt. Subi amesema katika kukabiliana na maambukizi mapya pamoja na utoaji wa elimu, wamezindua huduma za upimaji virusi vya ukimwi katika sehemu zote za huduma za afya ili kuwakinga watoto wanaozaliwa.
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa shirika la World Lung Foundation nchini Dkt. Nguge Mwakatundu amesema lengo la shirika hilo ni kupunguza vifo vya akinamama kwa asilimia kubwa, sambamba na kuwezesha asilimia themanini ya akinamama kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma.

