Msemaji wa polisi wa Indonesia, Anton Charliyan alisema kundi lenye uhusiano na IS huwenda lilihusika na shambulizi hilo na washambuliaji walionekana kujaribu kufuata mashambulizi ya ugaidi yaliyofanyika mwezi Novemba mjini Paris nchini Ufaransa.
Hata hivyo Shirika la habari la Aamag lenye uhusiano na wanamgambo wa Islamic State-IS lilisema shambulizi katika mtaa wa matajiri wa Jakarta liliyalenga mataifa ya kigeni na vikosi vya usalama vinavyofanya kazi kuwalinda.
Chanzo Voa
