Evod Mmanda
Sababu ya maamuzi hayo ni kutokana na eneo hilo kutokuwa makazi rasmi ya kuishi pamoja na kukosa kuwa na huduma za kijamii.
Agizo hilo amelitoa baada ya kufika katika kitongoji hicho, ambacho kipo pembezoni mwa Bahari ya Indi akiwa na kamati yake ya ulinzi na usalama, ambapo wananchi wake huishi katika nyumba za Makuti huku shughuli zao kuu zikiwa ni Uvuvi haramu.
Mwenyekiti wa Kitongoji hicho Juma Salum, amekiri kulipokea agizo la mkuu wa wilaya na kuahidi kulitekeleza huku baadhi ya wakazi wa kitongoji hicho akiwamo Hassan Mfaume akitii agizo.
Mkuu huyo wa wilaya amesema atarudi tena katika kitongoji hicho Aprili 9 kwa ajili ya kuangalia utekelezaji wa agizo lake.
Sikiliza



