Friday , 8th Jan , 2016

Chama cha Walimu mkoani Iringa(CWT), kimeitaka serikali mkoani Iringa kuyavunja mabaraza ya wafanyakazi yaliyokwishamaliza muda wake na kutendea haki kada ya ualimu kwa kuteua wajumbe wengi kutoka kada hiyo kama kanuni za utumishi zinavyoelekeza.

Mwenyekiti wa (CWT) mkoani wa Iringa Mwalimu, Stanslaus Muhongole

Mwenyekiti wa (CWT) mkoani humo Mwalimu Stanslaus Muhongole amesema kuwa mabaraza hayo yaliyokwishamaliza muda yanawanyima wafanyakazi haki ya kujumuika na hata uundwaji wa mabaraza hayo ulikiuka kanuni za utumishi kwa kuteua wajumbe wengi kutoka kada nyingine tofauti na ualimu.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho Samuel Muhaiki ameitaka serikali kuacha kulimbikiza madeni ya waalimu licha ya kuendelea kusuasua katika ulipaji wa deni la waalimu hao mkoa wa Iringa linalofikia zaidi ya shilingi milioni mia tisa

Naye mjumbe wa kamati tendaji ya CWT, Taifa anayewakilisha mkoa wa Iringa mwalimu Pius Kiwhele ameiomba serikali kupandisha kima cha chini cha mshahara wa walimu hadi shilingi laki sita ili kupunguza makali ya maisha kwa waalimu