Bunge la Seneti nchini Colombia
Makubaliano ya awali yalikataliwa kwa kura chache katika kura ya maoni iliyopigwa mwezi uliopita.
Rais wa nchi hiyo Juan Manuel Santos amesema mapendekezo mapya yana nguvu na yakizingatia madai ya mabadiliko yaliyotolewa na wapinzani.
Hata hivyo upande wa upinzani unaoongozwa na Rais wa zamani wa nchi hiyo Alvaro Uribe, amesema mapendekezo hayo yaliyofanyiwa mapitio bado hayakidhi matakwa ya viongozi wa FARC. mapendekezo hayo yanapelekwa bunge la chini kwa ajili ya kuidhinishwa.





