
Askofu mkuu wa kanisa katoliki jimbo kuu la Dar es salaam Kardinali Polycarp Pengo
Askofu Pengo ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati akiongea na East Africa Radio juu ya maoni yake kama kiongozi wa kanisa katoliki Dar es salaam moja ya makanisa yenye waumini wengi na kubwa duniani.
Katika hatua nyingine Kardinali Pengo ameitaka serikali isiruhusu siasa isiingilie suala la elimu kwani elimu ni msingi mkubwa wa kizazi cha sasa kinachokabiliwa na changamoto ya kuongezeka kwa maarifa.
Askofu Pengo ametoa rai hiyo mara baada ya kuzindua shule ya chekechea ya Santa Rita iliyojengwa na wahisani kutoka Italia na Sherehe zilizohudhuriwa na Balozi wa Italia hapa nchini Luigi Scotto ambaye pia ameendelea kusisitiza umuhimu wa elimu.