
Mkurugenzi Mkuu wa Twaweza, Aidan Eyakuze
Mkurugenzi mtendaji wa TWAWEZA Aidan Eyakuze amesema idadi hiyo ni ya wananchi kati ya 1,806 waliohojiwa Tanzania bara ambapo amesema asilimia 35 wamesema ubora wa elimu umebaki palepale na wengine asilimia 15 wamesema ubora umeshuka kabisa.
Vilevile asilimia 60 ya wananchi wameonesha kutamani kuwasomesha watoto wao katika shule binafsi.
Utafiti huo pia umebainisha kuwa asilimia 34 ya wananchi wamelalamikia ukosefu wa waalimu, asilimia 30 wamelalamikia ukosefu wa madawati na asilimia 13 wakilalamikia ukosefu wa madarasa, wengine wakilalamikia ufundishaji na ukosefu wa chakula kwa wanafunzi.
Adha tafiti hiyo pia imebaini kuwa asilimia 85 ya wazazi hawajihusishi na masuala ya masomo ya watoto wao, huku asilimia 83 imekuwa ni changamoto za miundombinu na matokeo mabaya ya wanafunzi na utovu wa nidhamu kwa wanafunzi
Utafiti huo umefanyika kati ya Agosti 7 na 14 mwaka huu hata hivyo baadhi ya wasomi walioshiriki uwasilishwaji wa ripoti hiyo kutoka chuo kikuu cha elimu wamesema matokeo hayo hayaendani na uhalisia wa hali ya elimu nchini na kwamba elimu haiwezi kuwa na ubora kwa kipindi cha mwaka mmoja pekee.