Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

VPL kuendelea tena leo, Azam mzigoni

Jumatatu , 22nd Feb , 2021

Klabu ya Azam 'Wanalamba lamba', wanatazamiwa kushuka dimbani saa 1:00 usiku wa leo tarehe 22 Februari 2021 kucheza dhidi ya TZ Prisons 'Wanajela jela' kwenye ligi kuu Tanzania bara mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Chamazi, jijini Dar es Salaam.

Wacheazaji wa Azam FC, Wakipongezana baada ya kufunga moja ya bao kwenye VPL msimu huu.

Kuelekea kwenye mchezo huo, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Zakaria Thabiti 'Zaka zakazi' amesema “Wachezaji wapo tayari kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya Prisons, tunawaheshimu wapinzani wetu ila nasi pia tupo tayari  ili kupata matokeo chanya ndani ya uwanja”.

Mchezo huo unatazamiwa kuwa wenye upinzani mkali kutokana na mahitaji ya alama 3 kwa timu zote mbili, lakini rekodi zinaonesha tokea wawili hao wakutane Oktoba 2012 wamecheza michezo 17, Azam akishinda 8, TZ Prisons akishinda 1 na sare 8.

Mara ya mwisho Wajela jela hao kuwafunga Azam ilikuwani tarehe 14 Februari mwaka 2019 ambapo walipata ushindi wa bao 1-0 kwenye dimba la sokoine jijini Mbeya na ndiyo mchezo pekee ambao Prisons wameifunga Azam ndani ya miaka 8 iliyopita.

Licha ya rekodi hiyo ya kibabe kwa wanalamba lamba hao, lakini rekodi za michezo mitano ya mwisho ya VPL wawili hao walipokutana, Azam alipata ushindi kwenye michezo miwili pekee, sare moja na kupoteza michezo miwili jambo linaloonesha upinzani mkali wa timu hizo kwa miaka ya karibuni.

Azam ipo nafasi ya tatu, wakiwa na alama 36, alama 13 nyuma vinara, klabu ya Yanga ilhali TZ Prisons ipo nafasi ya nane wakiwa na alama zake 25.

Mchezo mwingine wa VPL utakaopigwa hii leo, ni ule utakaowakutanisha timu ya Dodoma Jiji ambayo itawakaribisha Maafande kutoka mkoani Kilimanjaro, klabu ya Polisi Tanzania mchezo utakaochezwa saa 10:00 jioni kwenye dimba la Jamhuri jijini Dodoma.

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera