Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Usajili wa Ngoma, Azam FC yatoa neno kwa Yanga

Jumapili , 27th Mei , 2018

Klabu ya soka ya Azam FC ambayo jana imekamilisha usajili wa aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma, imerejesha shukrani kwa viongozi wa Yanga kwa kutoa ushirikiano na kufanikisha usajili huo.

Msemaji wa Azam FC Jaffar Idd Maganga, ameeleza kuwa viongozi wa Yanga wameonesha ukomavu mkubwa kwenye masuala ya michezo baada ya kubariki kwa asiliia zote uhamisho wa Ngoma kutoka kwenye klabu yao na kwenda Azam FC.

''Niwapongeze tu viongozi wa Yanga kwa kuweka wazi suala la usajili wa Ngoma kuwa walikuwa wamemalizana naye na taratibu zote zimefuatwa, ni jambo la kiungwana sana ambapo hata sisi tuliwahi kufanya hivyo kwenye usajili wa Gadiel Michael'', amesema.

Mbali na hilo Azam FC pia imeweka wazi kuwa usajili wa Ngoma ni mwanzo tu ila mashabiki wasubiri masika ya usajili yanayokuja ambapo timu yao itakuwa tishio msimu ujao wa 2018/19.

Azam FC kesho usiku itakuwa mwenyeji wa Yanga kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara, ambao utakuwa ni wa kufunga pazia la ligi msimu huu huku pia timu hizo zikiwania nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kuu.
 

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera