Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chaneta kubebwa kwa mbeleko

Ijumaa , 20th Mei , 2022

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi Pauline Gekul amesema kuwa Serikali itaendelea kuvibeba vyama vya michezo ikiwamo CHANETA kwa mbeleko mbili, moja ikiwa yake na ya pili ikiwa ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha michezo inaimarika nchini.

viongozi wa chama cha netiboli Tanzania.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Naibu Waziri Gekul Mei 20, 2022 akiwa njiani akitokea Babati mkoani Manyara kuja Dodoma kuendelea na shughuli zake za kikazi ikiwamo kufanya kikao na CHANETA ambacho ni Chama cha Mpira wa Netiboli nchini.

“Ninaposema mbeleko maana yangu kuwa mtoto anabebwa kwa ubeleko mmoja lakini pale kunapokuwa hakuna budi mama hufanya upendeleo wa kumbeba mtoto wake kwa mbeleko mbili kuhakikisha anafika mbali zaidi.”

Aliongeza kuwa yeye kwa ushirikiana na Waziri wake Mheshimiwa Mohammed Mchengerwa ubeleko wake umefungwa vizuri na vyama vya michezo vinakuwa imara na michezo inazidi kufanikiwa na ndiyo maana wamejiwekea utaratibu wa kukutana na vyama mbalimbali vya michezo kila mara.

“Ubeleko wa Rais Samia Suluhu Hassan katika michezo umekuwa imara zaidi kwa kuongeza bajeti ya michezo kila uchao.”

CHANETA wakiongoza na mwenyekiti wao Dkt. Devota Marwa wapo jijini Dodoma kwa ratiba maalumu ya mazungumzo ya kina na Serikali ambapo kwanza wameanzia na Bungeni ambapo walizungumza na wabunge wakiongozwa na watumishi kadhaa wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Wanatarajia kufanya kikao kizito na Naibu Waziri Gekul, ambapo CHANETA wanasema kuwa wamejindaa vema kuuboresha mchezo huo hapa nchini.

“Tumekamilika, uongozi wetu upo imara, tunahakika katika kikao hicho na serikali tutayaweka wazi mambo yetu kadhaa, tuna imani yatapokelewa kwa mikono miwili na mara zote Serikali imekuwa ikifanya hivyo.”

Katika kikao hicho CHANETA inaongozwa na viongozi wake 11 inayowajumuisha wanahabari wawili maarufu nchini Bi Shy-Rose Bhanji na Bi Betty Mkwasa.

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria