Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Lyon Vs Bayern rekodi za Bayern ni hatari

Jumatano , 19th Aug , 2020

Nusu fainali ya pili ya klabu bingwa barani ulaya Uefa Champions League itachezwa usiku wa leo katika dimba la Jose Alvalade ambapo Olympique Lyon ya Ufaransa wataminyana na Bayern Munich ya Ujerumani, mshindi wa mchezo huu atacheza fainali ya michuano hii na PSG Agosti 23.

Wachezaji wa Bayern Munich wakipongezana baada ya kufunga bao kwenye moja ya michezo ya ligi ya mabingwa.

Kocha wa Bayern Hansi Flick amewataka wachezaji wake kusahau ushindi wa mabao 8-2 walioupata kwenye mchezo uliopita wa robo fainali dhidi ya Barcelona watakapo wavaa Lyon usiku wa leo.

Katika hatua ya 16 bora Lyon iliitoa Juventus na ikaifunga Manchester City mabao 3-1 katika mchezo wa hatua ya robo fainali, hiyo kocha wa Bayern anaelewa hatari walionayo Lyon katika mchezo wa leo.

Rudi Garcia kocha wa Olympique Lyon anasema anajua kuwa Bayern ni timu hatari lakini rekodi hazina nafasi katika mchezo wa leo. Katika michezo tisa ya michuano hii msimu huu the Bavarians wamefunga mabao 39 huku wao wakiruhsu mabao 8 tu.

Kocha Garcia anasema Man City walifunga zaidi ya mabao 100 kwenye ligi kuu England EPL, anasema kama tunaangalia takwimu basi hawana budi kubaki hotelini na kuwaachana Bayern wacheze peke yao. Hatupewi nafasi lakini tumezitoa timu kubwa mpaka kufika hapa amesema Garcia

Bayern Munich na Lyon wanakutana kwa mara ya tisa kwenye michuano ya vilabu barani ulaya. Bayern wameshinda mara 4 na Lyon wameshinda mara 2 huku wakitoka sare mara mbili. Mara ya mwisho kukutana katika michuano hii ilikuwa katika hataua ya nusu fainali ambapo Bayern walipata ushindi wa jumla wa mabao 4-0 msimu wa 2009-10.

Hii ni mara ya 12 Bayern wanacheza katika hatua ya nusu fainali ya michuano hii, ni Real Madrid pekee ndio iliyocheza nusu fainali nyingi zaidi ya the Bavarians wao wamecheza mara 13.

Kocha Rudi Garcia anaweza kuwa kocha wa pili raia wa ufaransa kuipeleka timu katika hatua ya Fainali ya klabu bingwa ulaya endapo kama ataifunga Bayern Munich. Kocha pekee aliyewahi kufanya hivyo ni Didier Deschamps akiwa na kikosi cha Monaco Msimu wa 2003-03.

Kwenye michuano yote barani ulaya Bayern ndio timu iliyocheza michezo mingi mfululizo pasipo kupoteza. Wamecheza michezo 28 katika michuano yote wameshinda michezo 27 na wametoka sare mchezo mmoja.

Vikosi vinavyoweza kuanza katika mchezo huu kwa timu zote mbili.

Lyon: Lopes; Denayer, Marcelo, Marçal; Dubois, Caqueret, Guimarães, Aouar, Cornet; Depay, Dembélé

Bayern: Neuer; Kimmich, Boateng, Alaba, Davies; Goretzka, Thiago; Perišić, Müller, Gnabry; Lewandowski

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine