Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Hakuna mchezaji atakaa na kula pesa tu'' - Simba

Jumatano , 27th Jun , 2018

Klabu ya Simba kupitia kwa kocha wake Masoud Djuma, amesema katika usajili unaofanywa na timu yake hategemei kama kutakuwa na mchezaji atasajiliwa kwaajili ya kukaa na kusubiri mshahara tu.

Wachezaji wa Simba wakijadili jambo na kocha wao Masoud Djuma wakati wa mazoezi.

Masoud ameyasema hayo kwenye uwanja wa Boko Veteran jijini Dar es Salaam, ambako timu hiyo imeweka Kambi kwaajili ya maandalizi ya michuano ya Kombe la Kagame inayotarajiwa kuanza Juni 28.

''Huu mwaka tumesema hakuna mchezaji anasajiliwa Simba kuja kukaa benchi, atakaa benchi tu kwasababu kocha amefanya mabadiliko ya kikosi lakini hakuna mchezaji atakaa tu na kula mshahara, hilo hatulitaki'', amesema.

Masoud ameongeza kuwa michuano ya Klabu bingwa Afrika Mashariki na kati maarufu kama Kagame ataitumia kupima kikosi chake ili ajue naani atafaa kwenye eneo gani na endapo anakosekana mchezaji fulani asiwe na taabu kwenye kujua nani ataziba nafasi yake.

Simba ipo Kundi C  na timu za Singida United, APR ya Rwanda na Dakadaha ya Somalia. Simba itafungua dimba na timu ya Dakadaha Julai 30, Saa 10:00 jioni Uwanja wa Taifa. Hapo jana Simba imekamilisha usajili wa mshambuliaji Meddie Kagere kutoka Gor Mahia ya Kenya.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine