Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Shule 9 za Mtwara zilizopatiwa taulo za kike

Jumatano , 5th Oct , 2022

Mwezi Septemba mwaka huu kampeni ya Namthamini ilianza kugawa taulo za kike katika Mkoa wa Mtwara kwa lengo kuwasadia wanafunzi kubaki mashuleni kwa mwaka mzima na kupunguza changamoto wanazopata katika kipindi cha hedhi.

Mtangazaji wa East Africa TV, Najma Paul akifurahi na wanafunzi wa Masasi baada ya kumaliza kugawa taulo za kike katika shule hiyo.

Septemba 19 kampeni ya Namthamini ilianza katika Wilaya ya Mtwara kwa kugawa taulo za kike katika shule ya sekondari Mikindani walioungana na wanafunzi kutoka shule ya Sekondari Mitengo, ambapo jumla ya pakiti 862 za taulo za kike zilitolewa kwa wanafunzi shule hizo mbili, pamoja na kutoa elimu ya hedhi salama kwa wanafunzi wa kike na kiume.

Pia katika siku hiyo kampeni ya Namthamini iliendelea katika shule ya Sekondari Naliendele walioungana na wanafunzi kutoka shule ya sekondari Mangamba, ambapo jumla ya taulo za kike pakiti 969 zilitolewa kwa wanafunzi wa shule zote mbili.

Septemba 20 kampeni ya Namthamini iliendelea katika wilaya ya Masasi ambapo ilifika katika shule tatu za sekondari nazo ni Chiungutwa, Lukuledi na Masasi ambapo jumla ya taulo za kike pakiti 3048 zilitolewa kwa shule hizo tatu.

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Chiungutwa walipatiwa taulo za kike pakiti 1008

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Lukuledi walipatiwa taulo za kike pakiti 1056

Kampeni ya Namthamini wilaya ya Masasi ikamaliza kugawa taulo za kike katika wilaya hiyo katika shule ya Sekondari Masasi ambapo wanafunzi wa shule hiyo walipatiwa taulo za kike pakiti 984.

Septemba 21 kampeni ya Namthamini ikamaliza kugawa taulo za kike katika mkoa wa Mtwara katika wilaya ya Nanyumbu ambapo ilifika katika shule mbili za sekondari nazo ni Napacho na Nanyumbu.

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Napacho ilipatiwa taulo za kike pakiti 1050.

Kampeni ya Namthamini katika mkoa wa Mtwara ikamaliza kugawa taulo za kike katika shule ya Sekondari Nanyumbu ambapo jumla ya taulo za kike pakiti 1008 zilitolewa katika shule hiyo.

Kampeni ya Namthamini itaendelea kugawa taulo za kike mwezi Oktoba katika mikoa ya Njombe na Ruvuma.

HABARI ZAIDI

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera